sw_tn_fork/rev/20/11.md

823 B

Taarifa ya Jumla:

Hii ni sehemu ifuatayo ya maono ya Yohana. Anaelezea kuona ghafla kiti cheupe cha enzi na wafu wakihukumiwa.

Dunia na mbingu zilikimbia mbali kutoka katika uwepo wake, lakini hapakuwako nafasi ya wao kwenda

Yohana anaelezea mbingu na nchi kama vile ni watu wanaojaribu kutoroka hukumu ya Mungu. Hii inamaanisha kuwa Mungu aliaangamiza kabisa mbingu na nchi za zamani.

hodari na wasio wa muhimu

Yohana anaunganisha maneno haya yenye maana tofauti kumaanisha watu wote waliokufa.

vitabu vilifunuliwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mtu alivifunua vitabu"

Wafu walihukumiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu aliwahukumu watu waliokuwa wamekufa na sasa wako hai tena"

kwa kile kilichoandikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kwa kile alichoandika"