forked from WA-Catalog/sw_tn
29 lines
1.1 KiB
Markdown
29 lines
1.1 KiB
Markdown
# Taarifa ya Jumla:
|
|
|
|
Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.
|
|
|
|
# Zaburi ya Daudi
|
|
|
|
Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.
|
|
|
|
# Yahwe ni mchungaji wangu
|
|
|
|
Mwandishi anamzungumzia Yahwe kana kwamba alikuwa mchungaji. Hii inasisitiza jinsi Mungu anavyowajali watu kama mchungaji anavyowajali kondoo wake. "Yahwe ni kama mchungaji kwangu" au " Yahwe ananijali kama mchungaji anavyojali kondoo wake"
|
|
|
|
# sitapungukiwa kitu
|
|
|
|
Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nina kila kitu ninachohitaji"
|
|
|
|
# Ananifanya kulala chini kwenye malisho ya kijani
|
|
|
|
Mwandishi anajizungumzia kana kwamba ni kondoo, na anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni mchungaji. "Ananipa mapumziko kama mchungaji anavyowaongoza kondoo wake kulala chini kwenye malisho ya kijani"
|
|
|
|
# ananiongoza kando kando na maji yaliyotulia
|
|
|
|
Mwandishi anajizungumzia kana kwamba ni kondoo, na anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni mchungaji. "ananipa ninachohitaji kama mchungaji anayewaongoza kondoo wake kando kando ya maji matulivu"
|
|
|
|
# maji yaliyotulia
|
|
|
|
"maji yanayotiririka taratibu." Maji haya ni salama kunywa.
|
|
|