forked from WA-Catalog/sw_tn
1.0 KiB
1.0 KiB
Sentensi unganishi:
Yakobo anaendelea kuwaambia waamini wa Kiyahudi waliotawanyika namna ya kuishi kwa kupendana na kuwakumbusha kutowapendelea matajiri juu ya masikini.
Ndugu zangu
Yakobo anawaandikia ndugu zake ambao ni waamini wa Kiyahudi . "waamini wenzangu" au "ndugu zangu katika Kristo"
Ishikeni imani ya Bwana Yesu Kristo
Mwamini Yesu Kristo.
Bwana wetu Yesu Kristo
Neno "wetu" linamaanisha Yakobo na waamini wenzake.
upendeleo kwa watu wengine
shauku ya kumsaidia mtu fulani zaidi ya mwingine
Kama mtu fulani
Yakobo anaanza kuelezea hali ambayo waamini wanamthamini sana tajiri kuliko masikini.
amevaa pete za dhahabu na mavazi mazuri
"amevaa kama mtu tajiri"
keti hapa mahali pazuri
"keti hapa sehemu ya heshima"
simama pale
"hamia sehemu isiyo na heshima"
Kaa chini ya miguu yangu
Hamia sehemu ya kunyenyekea
Je, hamuhukumiani ninyi wenyewe, na kuwa waamuzi wenye mawazo mabaya?
Yakobo alitumia swali kuwakemea wasomaji wake. "Mnahukumiana wenyewe kwa wenyewe na kufanya maamuzi mkiwa na mawazo mabaya"