forked from WA-Catalog/sw_tn
824 B
824 B
Maelezo ya Jumla
Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.
enyi uharibifu wa Yerusalemu
Isaya anazungumzia uharibifu wa Yerusalemu kana kwamba ulikuwa mtu ambaye angeweza kushangilia. Hii inawakilisha watu wa Yerusalemu ambao walishindwa. "nyie watu ambao mnaishi miongoni mwa uharibifu wa Yerusalemu"
amemkomboa Yerusalemu
Hapa "Yerusalemu" inawakilisha watu. "amewakomboa watu wa Yerusalemu"
amafunua mkono wake mtakatifu
Hapa "mkono" inawakilisha nguvu ya Yahwe. Yahwe kuonyesha watu wote wa mataifa ya kwamba ni mtakatifu na mwenye nguvu inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa shujaa aliyetoa joho lake, kufunua mikono yake kwa ajili ya vita. "alionyesha utakatifu wake na nguvu yake kuu"
mataifa yote; dunia yote
Hapa "mataifa" na "dunia" inawakilisha watu wa mataifa yote katika dunia yote.