forked from WA-Catalog/sw_tn
21 lines
1.4 KiB
Markdown
21 lines
1.4 KiB
Markdown
# Jishangaze mwenyewe na ushangazwe
|
|
|
|
Neno "mwenyewe" lina maana ya watu wa Yerusalemu. Kwa nini wanashangazwa inawvza kuwekwa wazi. "Ushangazwe kwa kile nachotaka kukuambia"
|
|
|
|
# jipofushe na uwe kipofu
|
|
|
|
Watu kupuuza kile Yahwe anasema inazungumziwa kana kwamba wangeweza kujifanya vipofu wenyewe. "endelea kuwa mjinga na kipofu wa kiroho kwa kile nachokuonyesha"
|
|
|
|
# Lewa, lakini sio kwa divai; pepesuka, lakini sio kwa mvinyo
|
|
|
|
Watu kutokuwa na ufahamu na kutoelewa kile Yahwe anafanya inazungumziwa kana kwamba walikuwa wamelewa. "Uwe bila ufahamu kama mtu mlevi, lakini sio kwa sababu umekunywa divai au mvinyo kupitiliza"
|
|
|
|
# Kwa maana Yahwe amekumwagia juu yako roho ya usingizi mzito
|
|
|
|
Hapa " roho ya" ina maana "kuwa na sifa za" kuwa na usingizi. Yahwe kusababisha watu kuwa na usingizii inazungumziwa kana kwamba "roho" ilikuwa kimiminiko ambacho kilimwagwa juu ya watu. Pia "usingizi mzito" ni sitiari ambayo ina maana ya watu ambao hawana ufahamu na hawawezi kuelewa kile Yahwe anafanya. "Sababu hauna ufahamu ni kwa sababu Yahwe amesababisha uwe umelala kiroho"
|
|
|
|
# Ameyafumba macho yako, manabii, na amefunika vichwa vyako, watazamaji
|
|
|
|
Yahwe kusababisha watu kutokuwa na ufahamu na kutoelewa kile anachofanya inazungumziwa kana kwamba alifumba macho yao na kufunika vichwa vyao ili wasiweze kuona. "Ni kana kwamba Yahwe amefumba macho ya manabii na kufunika vichwa vya watazamaji"
|
|
|