1.2 KiB
Sentensi Unganishi
Baada ya salamu, Yohana anawaonyesha waumini kuwa upendo na kweli vinakwenda sambamba
Maelezo ya Jumla
Kihistoria mtume Yohana amekubalika kuwa ndiye mwandishi wa barua hii. Anasema "pendaneni" hii pengine barua hii liliandikiwa kanisa.
Maelezo ya Jumla
"ninyi" na "yenu" katika barua hii yanaonyesha wingi
Maelezo ya Jumla
katika barua hii Yohana anatumia maneno "sisi" na 'yetu" ikimaanisha Yohana mwenyewe pamoja na wasomaji wake
Kutoka kwa mzee kwenda kwa mwanamke mteule na watoto wake
Barua za wakati huo zilianza na jina la mwandishi, kwa kushupisha inaweza kusomeka:- " mimi, Yohana mzee, ninaandika barua hii kwa mwanamke mteule na watoto wake"
Mzee
Ni rejea kwa Yohana, mtume na mwanafunzi wa Yesu. Anajiita mzee labda kwa sababu ya umri wake mkubwa au kwa sababu ni kiongozi kanisani.
kwa mwanamke mteule na watoto wake
Pengine hii ina maana ya kundi au kusanyiko na waumini .
ambaye nampenda katika kweli.
" Ninyi watu ninaowapenda katika kweli"
wanao ifahamu kweli
"ambao wanao fahamu ukweli kuhusu Mungu na Yesu"
Baba...Mwana
Hivi ni vyeo muhimu vinavyoelezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu
katika kweli na upendo.
Neno "kweli" linaelezea "upendo." Pengine inamaanisha "katika upendo wa kweli"