sw_tn_fork/psa/107/011.md

880 B

waliasi dhidi ya neno la Mungu ... kukataa maagazi ya Aliye juu.

Misemo hii ina maana sawa na inasisitiza jinsi walivyomuasi Mungu, ambayo ndio sababu ya kufungwa.

Alinyenyekesha mioyo yao kupitia ugumu

Hapa moyo unamaanisha mtu, lakini mahususi mapenzi yake. "Aliwanyenyekesha kwa kuwaruhusu wapitie magumu"

ugumu

Maana zinazowezekana ni 1) "tabu" au 2) "kazi ngumu"

walijikwaa na hakuwepo mtu kuwasaidia kuinuka

Neno "kujikwaa" linamaanisha wakati watu hawa walijikuta kwenye nyakati ngumu sana. "waliingia taabuni na hakuwepo mtu wakuwakomboa"

Kisha wakamuita Yahwe katika tabu yao

Inaashiriwa kuwa wanaomba kwa Yahwe ili awasaidie. "Kisha wakaomba kwa Yahwe kuwasaidia katika shida yao"

dhiki yao

"taabu" au "mateso"

akawatoa

Hapa Daudi anaelezea Yahwe kuwaokoa kutoka dhiki yao kana kwamba dhiki ilikuwa sehemu ya kimwili ambayo alikuwa akiwatoa.