sw_tn_fork/psa/103/011.md

631 B

Kwa kuwa kama anga zilivyo juu ... kuelekea wale ambao humheshimu

Tashbihi inalinganisha umbali mkubwa kati ya mbingu na dunia kwa ukuu wa upendo wa Mungu kwa ajili ya watu wake.

Kama vile mashariki ilivyo mbali ... alivyoondoa hatia ya dhambi zetu kutoka kwetu

Umbali kati ya mashariki na magharibi ni mbali sana mpaka haiwezi kupimika. Katika tashbihi hii, umbali huo unalinganishwa kwa jinsi Mungu anavyosogeza mbali hatia yetu kutoka kwetu.

Kama vile baba alivyo na huruma ... juu ya wale amabo humheshimu

Hapa mwandishi analinganisha huruma ya baba kwa watoto wake kwa huruma ya Yahwe kwa wale ambao wanamheshimu.