\v 10 kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye? \v 11 Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka? \v 12 Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.