\c 23 \v 1 Mwanaume aliyejeruhiwa kwa kupondwa au kukatwa, haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la Yahwe. \v 2 Mwana haramu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.